Wednesday 7 September 2016

Zuberi

Ukiongelea kampuni nguli na mkongwe kwenye ruti ya DAR-MWANZA, huwezi ukamuacha Zuberi & Sons, kampuni hii imedumu miaka nenda rudi tangia kipindi kile cha Gonga shimo (Rough Road).

Enzi hizo Ukitoka Mwanza saa 12 asubuhi singida unafika saa 11 jioni,...

Kampuni hii imekua ikichepua kila siku wakianza na Masufuria(Local made bus) mpaka Andare na Volvo Bus. Baada ya kusoma upepo wa kibiashara Mzee Zuberi aliuza baadhi ya mabasi na kuhamia kwa mabasi ya kichina ili kwenda na wakati na soko la mabasi.

Kadri kampuni ilivyokuwa inakuwa kubwa, zikazaliwa kampuni nyingine pia kutoka Zuberi, ambazo ni Kisesa na Zube.

Kwa kwenda na TREND ya soko kampuni hii inamiliki basi kadha wa kadha za kichina ikiwa ni Higer na ZhongThong.

Kudhihirisha unguli wake wa kibiashara kampuni hutoa gari tano mpaka sita kwa ruti ya Dar - Mwanza ikiwa ni Mchanganyiko Zuberi na Kisesa.







No comments:

Post a Comment